DIRA (Vision)
Taarifa ya Maono hutoa mtazamo na mwelekeo wa baadaye wa Usharika ili kuwawezesha watumishi na Usharika
kwa ujumla kuweza kutekeleza majukumu yao kwa madhumuni waliyoyakusudia kwa pamoja.
Dira yetu kama Usharika ni:
Kukubali na kubadili Jamii yetu na ujumbe na upendo wa Yesu Kristo
Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kibamba lengo ni
kuwapa watu nafasi ya kumfahamu Yesu Kristo ili
kupata uzima wa milele. Kanisa limejengwa juu ya msingi wa Yesu Kristo, linaongozwa na Neno la Mungu kama linavyopatikana
Agano la Kale na Agano Jipya (Biblia ya Kikristo), na limeimarishwa katika misingi ya sakramenti. KKKT linaongozwa na Mkuu wa Kanisa (Askofu Mkuu) pamoja na Maaskofu kutoka dayosisi zote, wakisaidiwa na wakuu wa Majimbo
UJUMBE (Mission)
Taarifa ya ujumbe inafupisha lengo la kuwepo kwa Usharika na jinsi matarajio ya washarika yatakavyofikiwa.
Aidha ujumbe wa Usharika ni:
Kuwafanya watu wote kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo na kuwageuza watu wote kuwa wafuasi kamili wa Yesu Kristo
Pamoja na kuhakikisha Usharika wa Kibamba unakua endelevu na kupata mafanikio katika kutoa huduma ya Kichungaji kwa jamii, kuboresha Uinjilisti na huduma za misioni, uendelevu wa Kanisa pamoja na usimamizi bora wa rasilimali na miradi ya Usharika
MAADILI (Core Values)
Kazi ya Kanisa kwa ujumla inazingatiwa kwa maneno ya Yesu, 'Nenda ulimwenguni pote, na uhubiri injili kwa
viumbe vyote.
Mathayo 28: 18-20 Yesu akaja akawaambia, akisema, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, nendeni mkawafanye wanafunzi wa mataifa yote, na kuwabatiza kwa jina la Baba na wa Mwana na wa Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi, na tazama, mimi nipo pamoja nayi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Maadili yetu yanategemea imani, katika kuamini Biblia na Ulutheri na upendo wetu kwa Mungu na jirani
- Utukufu, huruma na haki (Dignity, compassion and justice)
- Msamaha na upatanisho (Forgiveness and reconciliation)
- Ujasiri na uwazi wa kubadilika (Courage and openness to change)
- Uaminifu wa uumbaji wa viumbe na zawadi za Mungu (Faithful stewardship of Gods creation and gifts)